Wednesday, July 13, 2016

VISANGA (VISA) lyrics by Bahati

Ni saa moja, na giza ya bisha
Hata bila kujulishwa, kila mtu nyumbani
Ni saa moja, na giza ya bisha
Mchunguze mwenzio, macho kwa telly, ooh
Visa vya anga, kila mtu yu kimya
Twangoja vidokezi ooh, huzuni wajaa hewani
Visa vya anga, kila mtu yu kimya
Twangoja vidokezi ooh, huzuni wajaa hewani
Na hakuna furaha, watu wajishika tama
Twalia kwa ndani, huzuni moyoni
Hakuna furaha, watu wajishika tama
Twalia kwa ndani, machozi moyoni

  (CHORUS)
Juu na visa ooh, vyatuvunja mioyo
Ukifungua macho hautamani, uonacho, ooh
Baba twajiweka, mikononi mwako
Juu machozi yetu, yamekuwa chakula chetu


Mara baba, kamshika mwanawe kwa nguvu
Mwingine kajitia kitanzi, baada ya mapenzi
Na yule, kasahau nduguye akifuata mali
Sasa ni upanga, kupigania shamba
Na hili halikosi, vita, kati ya dini
Hatuelewani, wakristo, waislamu
Kutwa kucha, tuko vitani Hatuelewi, hautelewi
Mara vita, mara ukabila, ya mataifa Hatuelewi, hatuelewi
Maskini walia hela, aliyenazo yualia amani
Hatuelewi, na hatuelewi

  (CHORUS)
Na visa ooh, vyatuvunja, mioyo
Ukifungua macho, hautamani uonacho
Ooh baba, twajiweka, mikononi, mwako
Juu machozi yetu, yamekuwa chakula chetu (x2)

No comments:

Post a Comment